News
TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI
TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI
Mkurugenzi wa Utafiti kwa niaba ya Bodi ya Wakurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Tumbaku Tanzania (TORITA) anapenda kuwataarifu Waombaji Kazi wote walioomba kazi ya Dereva kuwa usaili wa Vitendo unatarajiwa kuendeshwa Siku ya tarehe 20.12.2023 katika Ofisi ya Mkuu wa Usalama Barabarani – Mkoa wa Tabora na usaili wa mahojiano utafanyika siku ya tarehe 21.12.2023 TORITA - Tumbi kuanzia saa 2:00 Asubuhi na hatimaye kuwapangia kituo cha kazi waombaji kazi watakaofaulu usaili huo.
Wasailiwa wanaoitwa kwenye usaili wanapaswa kuzingatia maelekezo yafuatayo:-
- i.Kila Msailiwa anapaswa kuwa na kitambulisho kwa ajili ya utambuzi;
- ii. Vitambulisho vinavyokubalika ni pamoja na:- Kitambulisho cha Mkazi, Kitambulisho cha Mpiga kura,Kitambulisho cha kazi,Kitambulisho cha Uraia au Hati ya kusafiria.
- iii.Wasailiwa wanatakiwa kufika na VYETI VYAO HALISI, kuanzia cheti cha kuzaliwa, kidato cha IV, Vyeti vya mafunzo ya Udereva, Leseni na kuendelea kutegemeana na sifa za Mwombaji.
- iv. Wasailiwa watakaowasilisha Testimonials, Provisional Results, Statement of results, hatiza matokeo za kidato cha IV HAVITAKUBALIWA NA HAWATARUHUSIWA KUENDELEA NA USAILI.
- v.Kila msailiwa atajigharamia kwa Chakula, Usafiri na Malazi.
- vi.Kila Msailiwa azingatie tarehe, muda na mahali alipopangiwa kufanyia usaili.
- vii.Kwa waombaji waliosoma nje ya Tanzania wahakikishe Vyeti vyao vimehakikiwa na kuidhinishwa na Mamlaka husika (kama TCU, NACTE au NECTA)
- viii. Waombaji kazi ambao majina yao hayakuonekana katika tangazo hili watambue kuwa hawakukidhi vigezo. Hivyo, wasisite kuomba tena pindi nafasi za kazi zitakapotangazwa na kuzingatia mahitaji ya tangazo husika.
- ix.Msailiwa haruhusiwi kuja na simu au kifaa chochote cha kielekroniki kwenye eneo la usaili.
ORODHA YA MAJINA WALIOITWA KWENYE USAILI WA DEREVA
| | | | |
| | | | |
| | | | |
| | | | |
| | | | |
| | | | |
| | | | |
| | | | |
| | | | |
Imetolewa na,
Dkt. Jacob B. Lisuma
MKURUGENZI WA UTAFITI (TORITA)